Ufugaji wa Ng’ombe Tanzania

Ufugaji wa ng’ombe ni mkubwa sana kwa hapa Tanzania pia ngombe ni mifugo ambayo inategemewa sana na wananchi walio wengi hapa Tanzania.

Aina za Ngombe wa Tanzania

  • Ng’ombe wa Kisasa
  • Ng’ombe wa Kienyeji
  • Ng’ombe wa Chotara

Faida za ufugaji wa ng’ombe

  1. Ng’ombe hutupatia chakula kama vile maziwa na nyama
  2. Ng’ombe hutupatia mbolea
  3. Ng’ombe hutupatia ngozi ambayo hutumika kama malighafi kutengeneza, viatu, mikanda, mikoba, nguo na vitanda
  4. Ng’ombe hutupatia kujipatia pesa, pia ni akiba
  5. Ng’ombe hutupatia ni ufahari na huongeza heshima kwa baadhi ya makabila.
  6. Ng’ombe hutupatia mapambo kama pembe

Mambo Ya Kuzingatia Kwenye Ufugaji wa Ngombe

Baada ya kuchagua ngombe mzuri mambo mawili yafuatayo inabidi yazingatiwe;

  1. Chakula cha ng’ombe

Chakula ni kitu muhimu kwa ufugaji wa mifugo yote. Ulishaji wa ng’ombe wa maziwa na wengine huanzia  toka anapozaliwa (ndama) na ndipo atakapo kuwa na mafanikio mazuri katika uzalishaji.

Ndama anapozaliwa tu anahitaji kupata maziwa ya kwanza (colostrum) kwa muda usiopungua siku tatu mfululizo.

Maziwa haya humsaidia kujikinga na magonjwa na pia humpatia ndama virutubisho vya kutosha. Baada ya hapo ndama aendelee kunywa maziwa ya mama mpaka atakapofikia mwezi mmoja.

Baada ya mwezi aanze kupatiwa chakula cha ziada (pumba ya mahindi iliyochanganywa na mashudu  pamoja na majani mabichi yaliyokatwa katwa vipande vidogo vidogo).

Ndama akifikia umri kati ya miezi miwili na sita unaweza kumuachisha kunyonya, na anatakiwa apatiwe chakula chenye virutubisho sawa na maziwa ya mama.

Kwa mfano apatiwe pumba za mahindi zilizochanganywa na mashudu na majani mabichi (apatiwe wakati wote).

Ngombe jike wa kisasa hufikia umri wa kupandwa akiwa na mwaka mmoja na nusu.

Ng’ombe atakapokuwa na mimba ya miezi 7 kama alikuwa anakamuliwa anatakiwa kukaushwa na kupatiwa chakula chenye virutubisho zaidi.

  1. Banda La ng’ombe

Banda ni muhimu katika ufugaji wa ng’ombe. Tunashauriwa kuwahifadhi ng’ombe katika banda lenye  hewa ya kutosha, lisilo na joto kali, lisilopitisha maji ya mvua na liwe lenye nafasi ya kutosha.

Banda la ng’ombe inatakiwa iwe safi wakati wowote ili kuzuia magonjwa mbalimbali.

Pia banda la ng’ombe liwe na sakafu yenye mteremko kidogo kurahisisha usafi wa banda na kuzuia kutuama kwa maji na mkojo.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply