Ufugaji wa Vifaranga Vya Kuku Tanzania

Ufugaji wa vifaranga vya kuku wa kienyeji kwa Tanzania kuna mambo ya msingi ya kuzingatia na kwa kufanya hivyo kutakusadia sana kuweza kupata kuku kwa wingi.

Uandaaji wa Banda La Vifaranga

  1. Banda la vifaranga liwe safi, lisafishwe lisiwe na vumbi.
  2. Pulizia dawa ya kuondoa viroboto, utitiri na chawa kwa kutumia dawa kama Ectomin Dip.
  3. Pulizia dawa ya kudhibiti wadudu wasababishao magonjwa, tumia disinfectant mfano Vivid/TH4.
  4. Tayarisha taa na moto (charcoal) kwa ajili ya kuweka chumba kiwe na joto la kutosha.

Ufugaji wa Vifaranga Kwanzia Siku Ya Kwanza

SIKU YA 1.

  • Vifaranga wanapofika tu wapewe Glucose kwenye maji kwa masaa 8 mfululizo.
  • Baada ya hapo vifaranga vya kuku wapewe Vitalyte kwa siku 2 mfululizo.

SIKU YA 3.

  • Vifaranga wapewe chanjo ya Newcastle Vaccines kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatie Vitalyte au Antistress kwa siku 3 mfululizo.

SIKU YA 7.

  • Vifaranga wapewe chanjo ya Gumboro Vaccines kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatie maji ya Antistress kwa siku 2 mfululizo.

SIKU YA 10.

  • Wapatie vifaranga OTC Plus kwa siku kwa saa 24 kwa siku 3 mfululizo.

SIKU YA 14/18/19.

  • Wapatie vifaranga Esb3 na Vitalyte kwa masaa 24 kwa siku 3 mfululizo.

SIKU YA 21.

  • Vifaranga wanyweshe Newcastle Vaccines kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatie Antistress kwa siku 4 mfululizo.

SIKU YA 28.

  • Vifaranga wapewe Gumboro Vaccines kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo wapatie Antistress kwa siku 2 mfululizo.

SIKU YA 31.

  • Wapatie vifaranga OTC Plus kwa siku 7 mfululizo.

SIKU YA 43/44/45.

  • Wapatie vifaranga Esb3 na Vitalyte kwa masaa 24 mfululizo kwa siku 3.

SIKU YA 50.

  • Vifaranga wapewe chanjo ya Fowl Pox. Baada ya hapo endelea kuwapa Chickmycin au Chick Plus kwa wiki 2 mfululizo.

SIKU YA 65.

  • Wape vifaranga Chanjo ya Gumboro na baada ya hapo endelea na Antistress.

SIKU YA 69.

  • Vifaranga wapatie dawa ya Minyoo mfano Levalap kwa siku 2 mfululizo.

SIKU YA 72.

  • Vifaranga wapewe Fluquin kwa siku 5 mfululizo.

SIKU YA 79.

  • Vifaranga wapewe Anticox na Vitalyte kwa siku 5 mfululizo.

SIKU YA 90.

  • Vifaranga wapewe tena chanjo ya Newcastle Vaccines kwa saa 2 mfululizo. Baada ya hapo endelea kuwapa Antistress kwa siku 3 mfululizo.

Hapo sasa endelea na Utaratibu wa kawaida wa chanjo na tiba kwa vifaranga wako wa kuku.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

1 Comment
  1. Nataka nianzishe ufugaji wa vifaranga wa kienyeji kwahiyo naweza kuanza na vifaranga wangapi ambao wanauzwa Kwa bei Gani?

Leave a reply