Magonjwa Ya Nguruwe Na Dalili Zake

Magonjwa ya nguruwe ni changamoto katika ufugaji wa nguruwe na yamekuwa yakirudisha sana nyuma ufugaji wa nguruwe leo nimekuandikia magonjwa ya nguruwe pamoja na tiba zake.

Dalili za magonjwa ya nguruwe

  • Nguruwe haonyeshi dalili za kupenda chakula
  • Nguruwe Anaweza kuwa anahema kwa kasi
  • Nguruwe Anakua anajitenga
  • Macho makavu
  • Ngozi kavu
  • Masikio kulala 
  • Kwenye ngozi nyeupe ngozi inaweza kua nyekundu
  • Mkia kua mwembamba
  • Kuharisha mda mwingine kuhalisha damu

Chanzo Cha magonjwa ya nguruwe

Wadudu wa ndani

Minyoo ndio wadudu wakuu na huwa wanaathiri tumboni kwa nguruwe kwasababu tumboni kwa nguruwe kuna minyoo zaidi ya 30, ila minyoo ambao wanaathiri kwa wakati mwingi ni minyoo duara(round worm) na minyoo tape(tape worm).

1. Round worm

Hawa husababisha magonjwa ya nguruwe kwa sababu ukaa kwenye utumbo mpana wa nguruwe na uchukua chakula kutoka kwa nguruwe hivyo nguruwe anaweza kukonda. pia minyooo mikubwa (Ascaris lumbricoides) hii ndo inapatikana sana minyoo  hii ni mikubwa urefu wa penseli

Maambukizi yanaanza pale myama anapo kula chakula chenye mayai ya monyoo hao.

Dalili zake

  • Kunyonyoka manyoya(anorexia).
  • Upungufu wa damu(anaemia).
  • Baadae uzito upungua.

Kinga/Prevention

  • Kuzuia kwa kuweka dawa kwenye chakula na kutumia vyombo visafi
  • Kuchunga kwa kutumia njia ya mzunguko na kutibu nyasi
  • Kuwatenga watoto na wakubwa
  • Kuwapatia dawa ya minyoo mara kwa mara
  • Muoshe jike kabla ya kuzaa
  • Unaweza kutumia miti shamba aina ya moringa
2. Tape worm

Hawa husababisha magonjwa ya nguruwe wanakua flat kama rebon na wanapatikana mahali tofauti tofauti duniani. hawana utumbo hivyo wanakula kupitia ngozi yao na wanachukua virutubisho.

Huwa wanachukua folic acid na vitamin B-12 mwilini, wanaweza kusababisha sumu kwakua baada ya kula wanaacha uchafu na unakua kama mpira ambao unakaa karibu na ini.

Dalili zake

  • Kudumaa
  • Upungufu wa damu
  • Ngozi kubadilika nakua mbaya

KINGA/PREVENTION

  • Kuwapa dawa ya minyoo
  • Hakikisha wanao hudumia nguruwe wawe wanatumia choo na kusafisha

Wadudu wa nje

1. Mange

Ni moja ya magonjwa ya nguruwe ambayo Husababishwa na wadudu wanao itwa mites wanaishi kwenye ngozi ya nguruwe maeneo ya machoni, masikioni, miguuni na shingoni

Dalili zake

  • Nguruwe anakua anjikuna kuna kwenye ukuta kwenye miguu, macho na masikio
  • Ngozi inakua na mabaka kama vibarango na mistali mistali mwenkundu kama vidonda
  • Manyoya hua yamevurugika
  • Ngome anakua hatulii
  • Vifo
  • Kupungukiwa damu kwa watoto

Kinga/Prevention

  • Osha nguruwe mara mbili kwa wiki
  • Madume wanatakiwa kuoshwa pia
  • Wape dawa kila nguruwe anapoingia shambani kwako
  • Usafi wa banda

Tiba/Treatment

  • Unaweza kuwaosha  pia kwa maji safi na sabuni
  • Unaweza kuwaosha kwa organophosphate
  • Unaweza kuwachoma Ivermectin kwakua inasaidia sana
2. Chawa

Hawa husababisha magonjwa ya nguruwe kwakuwa wanakua wananyonya damu na dalili zake ni upungufu wa damu na pia mnyama anakua na madoa mekundu mwilini. Na pia unaweza kutibu Kwa kutumia viuadudu (insecticide) benzene hexachloride ndo hua inatumika kuua chawa.

3. Myiasis

Huu ni moja ya magonjwa ya nguruwe ni ugonjwa unaosababishwa na nzi wanao taga mayai kwenye vidonda, mayai hayo hukua hadi kufikia hatua ya kua nzi mkubwa na husababisha kidonda kua kikubwa zaidi.

Kidonda hua kichafu na kua kama na ukungu mweusi ambayo hayo ni mayai ya nzi, hivyo kuzuia hii unatakiwa kusafisha banda na kupunguza idadi ya nguruwe katika banda wasisongamane

Kinga/Prevention

Kuwapa Dawa za minyoo ambazo zimehakikishwa na ni salama pale zinapo pewa kutokana na maelekezo sahihi ni kamavermectin (Ivomec®), fenbendazole (Safe-Guard®), levamisole (Tramisol®, Levasole®), pyrantel (Banminth®), dichlorvos (Atgard®) na piperazine.

Unaweza kupanga ratiba ya kuwapa dawa zaminyoo na ukapanga na mtalaamu ili kua anawapa chanjo ifikapo siku sahihi

  • Dume/Boars – kila miezi 6 months
  • Jike/Sows – wiki 2 kabla ya kuzaa na baada ya kuwatenga watoto
  • Watoto/Piglets – wiki 1 baada ya kuwatenga
  • Wanao nenepeshwa/Fatteners – wiki moja baada ya kuwatenga na miezi mitatu badae
Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

6 Comments
  1. Asante sana kwa elimu uliyoitoa kwetu wafugaji

  2. Thanks alot, umenipa elimu nzuri sana ya haya magonjwa ya nguruwe.

  3. Asante sana kwa elimu nzuri kwasababu magonjwa ya nguruwe yanaleta sana hasara.

Leave a Reply to Lenald Minja Cancel reply