
Magonjwa ya nguruwe ni changamoto katika ufugaji wa nguruwe na yamekuwa yakirudisha sana nyuma ufugaji wa nguruwe leo nimekuandikia magonjwa ya nguruwe pamoja na tiba zake.
Dalili za magonjwa ya nguruwe
- Nguruwe haonyeshi dalili za kupenda chakula
- Nguruwe Anaweza kuwa anahema kwa kasi
- Nguruwe Anakua anajitenga
- Macho makavu
- Ngozi kavu
- Masikio kulala
- Kwenye ngozi nyeupe ngozi inaweza kua nyekundu
- Mkia kua mwembamba
- Kuharisha mda mwingine kuhalisha damu
Chanzo Cha magonjwa ya nguruwe
Wadudu wa ndani
Minyoo ndio wadudu wakuu na huwa wanaathiri tumboni kwa nguruwe kwasababu tumboni kwa nguruwe kuna minyoo zaidi ya 30, ila minyoo ambao wanaathiri kwa wakati mwingi ni minyoo duara(round worm) na minyoo tape(tape worm).
1. Round worm
Hawa husababisha magonjwa ya nguruwe kwa sababu ukaa kwenye utumbo mpana wa nguruwe na uchukua chakula kutoka kwa nguruwe hivyo nguruwe anaweza kukonda. pia minyooo mikubwa (Ascaris lumbricoides) hii ndo inapatikana sana minyoo hii ni mikubwa urefu wa penseli
Maambukizi yanaanza pale myama anapo kula chakula chenye mayai ya monyoo hao.
Dalili zake
- Kunyonyoka manyoya(anorexia).
- Upungufu wa damu(anaemia).
- Baadae uzito upungua.
Kinga/Prevention
- Kuzuia kwa kuweka dawa kwenye chakula na kutumia vyombo visafi
- Kuchunga kwa kutumia njia ya mzunguko na kutibu nyasi
- Kuwatenga watoto na wakubwa
- Kuwapatia dawa ya minyoo mara kwa mara
- Muoshe jike kabla ya kuzaa
- Unaweza kutumia miti shamba aina ya moringa
2. Tape worm
Hawa husababisha magonjwa ya nguruwe wanakua flat kama rebon na wanapatikana mahali tofauti tofauti duniani. hawana utumbo hivyo wanakula kupitia ngozi yao na wanachukua virutubisho.
Huwa wanachukua folic acid na vitamin B-12 mwilini, wanaweza kusababisha sumu kwakua baada ya kula wanaacha uchafu na unakua kama mpira ambao unakaa karibu na ini.
Dalili zake
- Kudumaa
- Upungufu wa damu
- Ngozi kubadilika nakua mbaya
KINGA/PREVENTION
- Kuwapa dawa ya minyoo
- Hakikisha wanao hudumia nguruwe wawe wanatumia choo na kusafisha
Wadudu wa nje
1. Mange
Ni moja ya magonjwa ya nguruwe ambayo Husababishwa na wadudu wanao itwa mites wanaishi kwenye ngozi ya nguruwe maeneo ya machoni, masikioni, miguuni na shingoni
Dalili zake
- Nguruwe anakua anjikuna kuna kwenye ukuta kwenye miguu, macho na masikio
- Ngozi inakua na mabaka kama vibarango na mistali mistali mwenkundu kama vidonda
- Manyoya hua yamevurugika
- Ngome anakua hatulii
- Vifo
- Kupungukiwa damu kwa watoto
Kinga/Prevention
- Osha nguruwe mara mbili kwa wiki
- Madume wanatakiwa kuoshwa pia
- Wape dawa kila nguruwe anapoingia shambani kwako
- Usafi wa banda
Tiba/Treatment
- Unaweza kuwaosha pia kwa maji safi na sabuni
- Unaweza kuwaosha kwa organophosphate
- Unaweza kuwachoma Ivermectin kwakua inasaidia sana
2. Chawa
Hawa husababisha magonjwa ya nguruwe kwakuwa wanakua wananyonya damu na dalili zake ni upungufu wa damu na pia mnyama anakua na madoa mekundu mwilini. Na pia unaweza kutibu Kwa kutumia viuadudu (insecticide) benzene hexachloride ndo hua inatumika kuua chawa.
3. Myiasis
Huu ni moja ya magonjwa ya nguruwe ni ugonjwa unaosababishwa na nzi wanao taga mayai kwenye vidonda, mayai hayo hukua hadi kufikia hatua ya kua nzi mkubwa na husababisha kidonda kua kikubwa zaidi.
Kidonda hua kichafu na kua kama na ukungu mweusi ambayo hayo ni mayai ya nzi, hivyo kuzuia hii unatakiwa kusafisha banda na kupunguza idadi ya nguruwe katika banda wasisongamane
Kinga/Prevention
Kuwapa Dawa za minyoo ambazo zimehakikishwa na ni salama pale zinapo pewa kutokana na maelekezo sahihi ni kamavermectin (Ivomec®), fenbendazole (Safe-Guard®), levamisole (Tramisol®, Levasole®), pyrantel (Banminth®), dichlorvos (Atgard®) na piperazine.
Unaweza kupanga ratiba ya kuwapa dawa zaminyoo na ukapanga na mtalaamu ili kua anawapa chanjo ifikapo siku sahihi
- Dume/Boars – kila miezi 6 months
- Jike/Sows – wiki 2 kabla ya kuzaa na baada ya kuwatenga watoto
- Watoto/Piglets – wiki 1 baada ya kuwatenga
- Wanao nenepeshwa/Fatteners – wiki moja baada ya kuwatenga na miezi mitatu badae
Asante sana kwa elimu uliyoitoa kwetu wafugaji
Asante sana boss
Thanks alot, umenipa elimu nzuri sana ya haya magonjwa ya nguruwe.
Asante sana Jumanne kwa comment yako na mimi nimefurahi kusikia hivyo.
Asante sana kwa elimu nzuri kwasababu magonjwa ya nguruwe yanaleta sana hasara.
Asante sana Engerasia kwa comment yako na nimefurahi sana kuiona pia ni kweli magonjwa ya nguruwe yanavunja sana moyo.