Kilimo Cha Mahindi Tanzania

Kilimo cha mahindi ni kilimo maarufu sana kwa Tanzania na zao hili lina faida nyingi sana kwasababu hutumika kwa chakula na pia hutumika kwa biashara

Maelezo Ya Kilimo Cha Mahindi

  • Mahindi ni zao muhimu linalo limwa katika maeneo ya kitropiki.
  • Udongo unaokubali zaidi ni wenye uchachu pH 6-6.5
  • Mahindi hustawi zaidi kwenye maeneo yenye mwinuko wa 2500

Jinsi Ya Kuandaa Shamba La Mahindi

  • Tayarisha shamba la mahindi mara tu baada ya kuvuna mazao ya msimu uliopita.
  • Mahindi hustawi sehemu yenye udongo wenye rutuba na usiosimamisha maji.
  • Moto usitumike wakati wa kuandaa shamba.

Faida za Kuandaa Shamba Mapema

  • Baada ya kuvuna,udongo bado ni mlaini hivyo hulimika kwa urahisi kwa kutumia jembe lolote.
  • Masalia yatakayofunikwa udongoni huoza mapema.
  • Hupunguza magugu.
  • Hupunguza wadudu waharibifu

Jinsi Ya Kupanda zao La Mahindi

Kupanda zao la mahindi mapema ni jambo muhimu kwani uwezekano wa kuvuna mazao mengi huwa ni mkubwa zaidi.

Kwa mashamba makubwa sana wakati wa kupanda uwe wiki moja kabla ya mvua kuanza kunyesha na isizidi wiki mbili kabla ya mvua.

isiwe mapema zaidi kwani mbegu zitaharibiwa na joto kati ya udongoni wadudu,panya,ndege na wanyama wengineo.

Faida za Kupanda Mahindi Mapema

  1. Mahindi yanapata mvua ya kutosha hadi kukomaa.
  2. Magonjwa hayatatokea au yatakuwa kidogo.
  3. Mbolea uliyoweka itayeyuka pamoja na mahindi yastawi vizuri.

Mbegu Bora za Mahindi

Mbegu bora ni zile zilizo zalishwa kitaalamu.

Faida za Kuchagua Mbegu Bora

  • Ni safi hazijabunguliwa na wadudu.
  • Huzaa mazao mengi.
  • Hustahimili magonjwa.

Aina za Mbegu za Mahindi

  1. Mbegu aina ya chotara (hybrid)
  2. Aina ya ndugu moja (synthetic)
  3. Mbegu aina ya composite

Mbegu za kisasa zikitumiwa vizuri katika misingi ya kilimo zina uwezo wa kuzaa magunia 50-80 au tani 5.5 – 7.5 kwa hekta moja au umi kwa hekari.

Mbegu Bora za Kupanda

Kuna mbegu nyingi za kisasa zilizoko kwenye soko mfano wa SIDCO ,PANNAR, CHOTARA, kutoka KENYA n.k

Kiwango Cha Mahindi Katika Eneo

Idadi ya mimea katika eneo ni muhimu kwani ikazidi

  • Kuna uwezekano wa mazao hupungua.
  • Mmea huangushwa na upepo
  • Mabua mengi hayazai.

Idadi ya mimea nayo ikipungua kwenya eneo husababishwa mavuno kupungua jambo la kufanya ni kupanda mbegu katika nafasi sahihi zilizoshauriwa na wataalamu.

Kiasi Cha Kupanda Mahindi

  • Mbegu za mahindi huhifadhiwa kwa dawa kali (sumu)
  • Kiasi cha kilo 20 za mbegu kinatosha kupanda hekari moja (Hii hutegemea na aina ya mbegu)

Nafasi za kupanda Mahindi

  • 75cm x 30cm
  • 75cm x 60cm
  • 90cm x 25cm
  • 90cm x 50cm

Uwekaji wa Mbolea Kwenye Mahindi

Mahindi hustawi na kuzaa vizuri iwapo yatapatiwa mbolea pamoja na matunzo mengine ya kilimo bora. 

Hata ukipanda mbegu bora bila kutumia mbolea ni kazi bure.

Aina za Mbolea za Mahindi

1. Mbolea za Asili

Samadi, mboji na majani mabichi,mbolea hizi hua na virutubisho vya kutosh ambavyo havijulikani vipo kwa kipimo kiasi gani.

2. Mbolea za Viwandani

Hizi hua na virutubisho vya kutosha na vipimo hujulikana, hii inasaidia kujua ni kiasi gani kitumike kwa kipindi gani.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply