Mwanzo wa Kilimo Bora Cha Viazi Vitamu Tanzania

Viazi vitamu ni moja kati ya mazao makuu ya mizizi Kutokana na uwezo wake wa kuvumilia ukame, zao hili la viazi vitamu ni moja kati ya mazao ya kinga ya njaa

Hapa nchini zao hili la viazi vitamu hulimwa zaidi katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Dodoma, Morogoro, Kagera, Arusha na Ruvuma.

Kuna aina mbalimbali za viazi vitamu zikiwemo Ukerewe, Kakamega, Karoti C, Mavuno, Pananzala na Polista.

Zao la viazi vitamu hustawi maeneo mengi hapa nchini na hukubali vizuri zaidi katika maeneo ya tambarare yenye udongo tifutifu ambao unaruhusu maji kupenya kirahisi.

Udongo mfinyazi na wenye kokoto nyingi haufai kwa ajili ya kilimo cha viazi vitamu kwasababu huzuia mizizi kupenya na kupanuka.

Kabla ya kuanza rasmi kilimo cha viazi vitamu, mkulima anapaswa kuhakikisha shamba linatayarishwa vizuri kwa kufyeka vichaka na kung’oa visiki.

Pia majani yanatakiwa kufunikwa wakati wa kutengeneza matuta ili kuongeze rutuba.

Wataalamu wanashauri kupanda viazi kwa kutumia mashina yenye urefu wa sentimita 30 kwa matokeo mazuri zaidi. Inashauriwa kutumia sehemu ya juu ya shina kuongeza mavuno.

Mashina yanatakiwa kupandwa katika umbali wa sentimita 25 hadi 30 kutoka mmea hadi mmea na sentimita 60 hadi 75 kutoka tuta hadi tuta.

Viazi pia vinaweza kupandwa kwa kutumia viazi vyenye afya na vyenye uzito wa gramu 20 mpaka 30.

Uandaaji wa Shamba La Viazi Vitamu

Mkulima anatakiwa kupalilia shamba miezi miwili ya mwanzo ili kuwezesha mmea kutambaa vizuri. Baada ya muda huo, viazi huweza kufunika ardhi na hivyo huzuia uotaji wa magugu.

Changamoto za Kilimo cha Viazi Vitamu

Wadudu kama vile kipepeo, mbawa kavu, fukusi na minyoo fundo ni baadhi ya changamoto za aina hii ya kilimo. Viazi vitamu pia hushambuliwa na magonjwa mbalimbali yatokanayo na virusi.

Magonjwa haya pamoja na uwepo wa wadudu yanaweza kudhibitiwa kwa usafi, kubadilisha mazao pamoja na kuzingatia udhibiti sango.

Mavuno Ya Viazi Vitamu

Kilimo cha viazi vitamu ni kwamba huchukua muda mfupi tu kukomaa, hivyo mkulima anaweza kupata faida mapema. Mara nyingi viazi huwa tayari kuvunwa kuanzia miezi mitatu hadi minne tangu kupandwa kulingana na hali ya hewa.

Viazi huvunwa kidogo kidogo kwa kutumia mikono, vijiti, jembe au rato Pia Mkulima anatakiwa kuhakikisha viazi haviachwi ardhini kwa muda mrefu kwasababu vitakomaa kupita kiasi na kuharibu ubora wake.

Uvunaji unapaswa kufanywa kwa uangalifu mkubwa ili kuhakikisha viazi havikatwi wala kuchubuliwa wakati wa zoezi hili.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply

Wauzaji
Logo