Kilimo Cha Bilinganya Tanzania

Kilimo cha bilinganya ni kilimo kizuri kwa Tanzania pia zao la bilinganya huwapatia wakulima faida nzuri kwasababu bilinganya hutumiwa sana kwenye mapishi.

Zao la bilinganya huhitaji hali yajoto la wastani, udongo wenye kina kirefu na rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji.

Aina za Bilinganya

Aina za bilinganya zinazolimwa kwa wingi katika nchi za ukanda wajoto ni kama zifuatazo

1. Black Beauty

Aina hii huzaa sana, matunda yake meusi, makubwa, na ya mviringo.

2. Florida Market

Matunda ya Florida Market yana umbo la yai. Aina hii pia huzaa sana, lakini hushambuliwa kwa urahisi na ugonjwa wa mnyauko bakiteria (Bacterial wilt).

3. Florida High Bush

Matunda yake ni makubwa ycnye umbo la yai na rangi ya kijani kibichi iliyochanganyika na nyeusi.

4. Newyork Spineless

Matunda ya Newyork Spineless ni ya mviringo, makubwa na yana rangi ya zambarau.

5. Peredeniya

Aina hii huzaa sana, matunda yake ni makubwa kiasi na yana umbo la yai.

Aina zingine za bilinganya ni Matale, Kopek na Rosita. Aina hizi huvumilia sana mashambulizi ya ugonjwa wa mnyauko bakteria.

Jinsi Ya Kuotesha Mbegu za Bilinganya

Mbegu za bilinganya huoteshwa kwanza kwenye kitalu na baadaye miche huhamishiwa shambani. Kabla ya kusia mbegu, tengeneza tuta lenye upana wa mita moja na urefa wowote.

Weka mbolea za asili kama vile samadi au takataka zilizooza vizuri, kiasi cha ndoo moja au mbili katika eneo la mita mraba moja.

Sia mbegu za bilinganya kiasi cha gramu mbili mpaka tatu (nusu kijiko cha chai chenye ujazo wa gramu tano) katika eneo hilo.

Gramu 500 za mbegu zinatosha kupandikiza katika eneo la hekta moja. Nafasi kati ya mstari na mstari iwe sentimita 10 hadi 15, na kina kiwe sentimita 1.5.

Baada ya kusia mbegu fukia na tandaza nyasi kavu na kisha mwagilia maji. Endelea kumwagilia kitalu kila siku, asubuhi najioni, hadi mbegu zitakapoota.

Mbegu za bilinganya huota baada ya siku 10 hadi 12.

Jinsi Ya Kuhamisha Miche Ya Bilinganya

Miche huwa tayari kwa kupandikizwa shambani baada ya wiki sita hadi nane. Wakati huu huwa na urefu wa sentimita 15 mpaka 20 (sawa na urefu wa kalamu ya risasi).

Mwezi mmoja kabla ya kupandikiza miche, rutubisha udongo kwa kuweka mbolea za asili zilizooza vizuri. Mbolea hizi ni kama samadi, mbolea vunde na mbolea ya kuku.

Weka kiasi cha tani 10 hadi 20 kwa hekta. Kiasi hiki ni sawa na kuweka ndoo moja hadi mbili zenye ujazo wa lita 20 katika eneo la mita mraba moja.

Mbolea ya mchanganyiko aina ya N.P.K yenye uwiano wa 20:10:10 huwekwa kwenye shimo wakati wa kupandikiza mche.

Kiasi kinachohitajika ni gramu tatu hadi tano (sawa na nusu kijiko mpaka kijiko kimoja kidogo cha chai) kwa kila shimo.

Jinsi Ya Kupandikiza Bilinganya

Aina ndogo za bilinganya hupandikizwa katika nafasi ya sentimita 80 mpaka 100 kutoka mstari hadi mstari na sentimita 50 mpaka 60 kutoka mche hadi mche.

Aina kubwa hupandikizwa katika nafasi ya sentimita 80 mpaka 100 kutoka mstari hadi mstari na sentimita 80 mpaka 90 kutoka mche hadi mche.

Kazi ya kuhamisha miche ifanyike kwa uangalifu mkubwa ili kuepuka kuikata mizizi.

Jinsi Ya Kutunza Shamba La Bilinganya

1. Jinsi Ya Kuweka Matandazo

Mara baada ya kupandikiza miche, tandaza nyasi kavu. Matandazo husaidia kuhifadhi unyevu, huzuia magugu yasiote na huongeza rutuba ya udongo.

2. Jinsi Ya Kufanya Palizi

Hakikisha shamba ni safi wakati wote ili kuzuia ushindani wa chakula, maji na mwanga kati ya mimea na magugu.

Usafi wa shamba pia huondoa maficho ya wadudu waharibifu na huzuia kuenea kwa magonjwa.

3. Jinsi Ya Kuweka Mbolea

Mbolea ya kukuzia aina ya S/A huwekwa wiki tatu baada ya mmea kuanza kutoa maua. Kiasi cha gramu tatu hadi tano huwekwa kuzungukia kila mche.

Mbolea iwekwe katika umbali wa sentimita tano mpaka 15 kutoka kwenye shina, kutegemea ukubwa wa mche.

Hakikisha mbolea haigusi mmea.

4. Jinsi Ya Kukata Kilele

Wiki mbili baada ya kupandildza miche, kata sehemu yajuu ya mmea (kilele) kama umepanda aina ndefu ya bilinganya.

Hii itasaidia kupata matawi matatu hadi manne na mmea kutengeneza umbile la kichaka. Matawi yakizidi manne yaondolewe ili kupata mazao mengi na bora.

5. Jinsi Ya Kumwagilia Bilinganya

Zao la bilinganya hustawi vizuri likipata maji ya kutosha. Umwagiliaji ufanyike kila siku asubuhi na jioni kutegemea hali ya hewa.

Wadudu Waharibifu wa Bilinganya

1. Wadudu wa Vinyatomvu

Wadudu hawa hushambulia zaidi sehemu ya chini ya jani. Hufyonza utomvu wa majani na kusababisha majani kuwa na mabaka meupe au njano.

Mashambulizi yakizidi majani huanguka chini. Vinyatomvu wanaweza kuzuiwa kwa kunyunyizia moja ya dawa zifuatazo

  • Deltamethrin (Decis)
  • Dimethoate (Sapa Dimethoate)
  • Fenvalerate (Sumicidin)
  • Lambda – Cyhalothrin (Karate).

2. Wadudu wa Vidukari

Hawa ni wadudu wadogo wenye rangi nyeusi. Hushambulia majani machanga na kuyasababisha kudumaa na kukunjamana.

Zuia wadudu hawa kwa kutumia mojawapo ya dawa zifuatazo

  • Dimecron 50% E.C
  • Lambda
  • Cyhalothrin (Karate)
  • Dichlorvos (Nogos)

3. Wadudu wa Utiriri wa Mimea

Ni vidudu vidogo vyenye rangi nyekundu iliyoiva pia hushambulia majani kwa kufyonza utomvu na majani yaliyoshambuliwa huonyesha utando kama wa buibui.

Mashambulizi yakizidi mmea hudumaa, majani hukauka na hatimaye hufa pia utiriri unazuiwa kwa kutumia dawa zifuatazo

  • Acrex
  • Karathane 25% W.P
  • Dimethoate
  • Ekalux
  • Kelthane.

4. Wadudu wa Minyoo Fundo

Wadudu hawa hushambulia mizizi. Hutoa kinyesi ambacho ni sumukwammea. Sumu hii husababisba mizizi kuwa na nundu kama ya mizizi ya maharagwe.

Mashambalizi yakizidi mmea hudumaa, hunyauka na hatimaye hufa pia njia ya kuzuia wadudu hawa ni kubadilisha mazao.

Kwa mfano; baada ya kuvuna zao hili, zao linalofuata lisiwe lajamii moja na bilinganya, kamavile nyanya, pilipili naviazi mviringo.

Pia dawa aina ya Carbofuran (Furadan) inaweza kutumika.

Magonjwa Yanayo Haribu Biliganya

1. Ugonjwa wa Mnyauko Bakteria

Ugonjwa huu husababishwa na backteria. Mmea ulioshambuliwa hunyauka ghafla hasa wakati wajua kali
Mnyauko bakteria unaweza kuzuiwa kwa kubadilisha mazao shambani.

Endapo ardhi itashambuliwa na ugonjwa huu zao la bilinganya lisipandwe katika eneo hilo kwa muda wa miaka mitatu hadi mitano.

Njia nyingine ni kupanda aina za bilinganya kama vile Matale, Kopek, na Rosita ambazo huvumilia mashambulizi ya ugonjwa huu.

2. Ugonjwa wa Phomopsis Vexans

Ugonjwa huu husababishwa na bakteria na hushambulia majani, shina na matunda.

3. Ugonjwa wa Verticillium Wilt

Huenezwa na maji na husababisha mmea kudumaa, majani kukunjamana na kuanguka.

Magonjwa ya Phomopsis Vexans na Verticillium Wilt yanaweza kuzuiwa kwa kung’oa na kuchoma moto mimea iliyoshambuliwa, kubadilisha mazao, na kuweka shamba katika hali ya usafi wakati wote.

Jinsi Ya Kuvuna Bilinganya

Bilinganya huanza kutoa matunda yaliyokomaa baada ya miezi miwili hadi mitatu tangu kupandikiza.

Uvunaji huendelea kwa muda wa zaidi ya miezi minne na hauna budi ufanyike mapema mara matunda yanapokomaa.

Matunda yaliyokomaa sana hayafai kuliwa kwa sababu huwa na kambakamba na mbegu zilizokomaa. Vuna mara mbili au tatu kwa wiki, kwa kutumia kisu kikali ili usiumize matunda.

Mavuno Ya Bilinganya

Kwa kawaida zao hili huzaa sana iwapo limetunzwa vizuri. Shamba lililotunzwa vizuri linaweza kutoa mavuno tani 50 hadi 60 kwa hekta.

Hata hivyo mavuno mengi hutegemea aina ya bilinganya, umwagiliaji na rutuba ya udongo.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply