Kilimo Cha Viazi Mviringo Tanzania

Kilimo cha viazi mviringo ni kilimo kizuri kwa Tanzania kwasababu viazi mviringo ni moja ya mazao muhimu katika mazao ya mizizi.

Mambo Muhimu Katika Kilimo Cha Viazi

Ubora wa zao la viazi mviringo hutegemea sana matunzo ya zao hilo wakati wa uzalishaji. Viazi vinavyopata matunzo mazuri hutoa mazao yenye ubora unaotakiwa katika hifadhi ya muda mrefu na usindikaji.

Jinsi Ya Kuchagua Mbegu Ya Viazi

Chagua aina ya mbegu kufuatana na mahitaji ya soko na nayovumilia mashambulizi ya magonjwa. Tumia mbegu bora isiyo na magonjwa na inayozaa mazao mengi na bora.

Jinsi Ya Kuweka Mbolea Kwenye Viazi

  • Viazi vitamu vinahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao mengi na bora.
  • Tumia mbolea za asili ili kudumisha rutuba.
  • Utayarishaji, Hifadhi na Usindikaji wa Mazao ya Mizizi baada ya Kuvuna.
  • iwapo ni lazima kutumia mbolea za viwandani ni muhimu kupata ushauri wa
  • Kitaalam kuhusu aina na viwango vya mbolea.

Jinsi Ya Kupalilia Viazi Mviringo

Palilia ili kuondoa magugu na kuruhusu mimea kutumia unyevu na rutuba vizuri pia wakati wa palizi pandishia udongo kwenye mimea ili kuepusha jua linaloweza kushusha ubora wa zao.

Viazi vilivyopigwa na jua hubadilika rangi na kuwa vya kijani na ubora hushuka. Viazi vya namna hii huwa havihifadhiki kwa muda mrefu.

Jinsi Ya Kupanda Viazi Mviringo

Ni muhimu kuzingatia nafasi ya kupanda ili kupata mazao mengi na bora pia panda kwa nafasi kama inavyoshauriwa na wataalamu.

Jinsi Ya Kudhibiti Magonjwa

Zao la viazi mviringo huathirika kwa urahisi na magonjwa ya ukungu, bakteria na virusi ambavyo visipodhibitiwa huweza kuleta hasara kubwa kuanzia shambani hadi ghalani.

Hivyo muhimu kukagua shamba la viazi mviringo ili kubaini na kudhibiti magonjwa kabla ya kusababisha upotevu wa zao.

Maandalizi Kabla Ya Kuvuna

Ni muhimu kufanya maandalizi ya kutosha ili kupunguza upotevu wa mazao.

Jinsi Ya Kukagua Shamba La Viazi Mviringo

Kagua shamba kuona kama viazi mviringo vimekomaa. Viazi mviringo hukomaa kati ya miezi mitatu hadi minne toka kupanda.

Dalili za Viazi Mviringo Vilivyokomaa

  • Udongo uliozunguka shina hupasuka
  • Majani hubadilika rangi kutoka kijani kuwa ya manjano.
  • Mizizi midogo midogo ya viazi hunyauka.
  • Sehemu ya juu ya mmea hunyauka.

Vifaa Vya Kuvunia Viazi Mviringo

  •  Majembe
  •  Magunia
  •  Vikapu

Usafiri wa Kusafirisha Viazi Mviringo

  •  Magari
  •  Matela ya matrekta
  •  Mikokoteni

Vifungashio vya Viazi Mviringo

  •  Magunia

Jinsi Ya Kuvuna Viazi Mviringo

Viazi mviringo huweza kuvunwa kwa kutumia jembe la mkono na jembe maalum la kukokotwa na wanyama.

Ni muhimu kuvuna wakati kuna unyevu kiasi kwenye udongo ili kurahisisha uvunaji.

Jinsi Ya Kuvuna Kwa Kutumia Mikono

Mashina ya viazi mviringo yanaweza kung’olewa kwa mkono au kuchimbuliwa kwa jembe kutegemea hali ya udongo.

  • Uangalifu ni muhimu ili kuepuka kukata au kuchubua viazi.
  • Ng’oa viazi na kung’uta udongo
  • Viache shambani kwa muda wa siku moja ili vinyauke na kuimarisha ngozi.

Jinsi Ya Kuhifadhi Viazi Mviringo

Weka viazi mviringo kwenye magunia au kwenye vikapu na vipeleke sehemu ya kusafishia, kuchambulia na kufungashia.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply