Jinsi Ya Kuchagua Jina Zuri La Biashara Tanzania

Jinsi ya kuchagua jina la biashara tanzania na kuhakikisha jina la biashara yako linaendana moja kwa moja na biashara unayoifanya ukiwa tanzania

Mambo ya kuzingatia katika kuchagua jina la biashara

  1. Usichukue Maoni Ya Kila Mtu

Kwenye kuchagua jina la biashara Kila mtu huwa na mawazo yake hivyo mfanyabiashara akiruhusu maoni kutoka kwa wadau mbalimbali kufanya uamuzi sahihi itakuwa changamoto.

Badala ya kusikiliza maoni ya kila mtu unaweza kuunda kikundi kidogo cha watu wa aina mbalimbali ambao watakusaidia kufanya uamuzi sahihi na kukupatia ushauri.

Kufanya hivi kunarahisisha zoezi zima la kuchagua jina jina sahihi la biashara kwani maoni ni machache na hivyo yote yanaweza kuchambuliwa na kujadiliwa kwa umakini zaidi.

Unapofanya hivi hakikisha kundi hilo linajumuisha watu wa aina tofauti ili uweze kupata maoni ambayo hayafanani.

  1. Usiunganishe Maneno Mawili Kuwa Moja

Katika wa zoezi la uchaguzi wa jina la biashara unachotakiwa kufahamu ni kwamba kwa sababu una uwezo wa kuunganisha maneno pamoja haimaanishi kuwa unapaswa kufanya hivyo.

Mara nyingi majina ya biashara yaliyounganishwa yanachanganya hivyo ni rahisi kusahaulika. Inatakiwa kuwa mbunifu na kuhakikisha kuwa jina la biashara yako linaeleweka na haliwachanganyi wateja kwa namna yoyote ile.

  1. Hakikisha Jina La Biashara Yako ni La Kipekee na Lina Mvuto Kwa Wateja

Epuka Jina la biashara ambalo linaelezea kwa undani biashara yako inahusu nini moja kwa moja kwa kuwa mengi huwa marefu na hivyo kukosa ubunifu jambo ambalo linaweza kusababisha wateja wasivutiwe na hivyo kununua mahitaji yao sehemu nyingine.

Jina la biashara yako linatakiwa kuhamasisha wateja na sio kuwafukuza.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

2 Comments
  1. Je mtu akiandika mabecity katika biashara itafaa

Leave a Reply to Lenald Minja Cancel reply