
Faida za kutangaza biashara kwenye Mitandao ya kijamii?
- Gharama ya Kujitangaza ni ndogo sana
Gharama ya mitandao ya kijamii ni nafuu sana na programu nyingi za mitandao ya kijamii ni bure. Kutangaza kupitia mitandao ni rahisi mno ukilinganisha na njia za kawaida tulizo zoea.
- Inaongeza ufahamu wa biashara yako
Mitandao ya kijamii inaongeza uwezo wa ufahamu wa bidhaa na biashara yako kwa haraka Kwa Kutumia mitandao ya kijamii kwenye biashara yako kunakupa nafasi ya kujitambulisha kwa wateja wa biashara yako kwa haraka zaidi.
- Ni rahisi kutumia
Mitandao ya kijamii ni rahisi kutumia Pia unao uwezo wa kutumia popote ulipo endapo tu utakuwa na kifaa kinacho kuwezesha kuingia kwenye mitandao ya kijamii.
- Kuwafahamu washindani wako wa kibishara
Ikiwa unataka kubaki kwenye ushindani katika soko la digital ni muhimu kwamba uanze kufanya kazi ya kujenga uwepo wako kwenye mitandao ya kijami.
- Inaokoa Muda
Mitandao ya kijamii yanaokoa muda ukilinganisha na njia nyingine katika kutangaza biashara yako. Unaweza kuamua kutumia mitandao ya kijamii wakati wowote ule utakaoona unafaa. Hivyo basi haikupi masharti ya muda na wakati maalumu wa kuyaendesha matangazo yako.
Asante kwa maelezo mazuri na faida zake.
Asante sana boss.
Kweli mitandao ya kijamii ina faida kubwa sana katika biashara
Faida za mitandao ya kijamii kwenye biashara ni nyingi sana boss.