Faida za Kusema Hapana Kwenye Maisha

Kwenye maisha yetu ni muhimu sana kusema Hapana na tunatakiwa kufanya maamuzi fulani ya kukataa na sio kukubaliana kila mipango au jambo.

1. Kusema Hapana Hukutenga na Mipango Mibaya

Siyo kila mpango unafaa kwenye maisha yako. Mipango mingine inaweza kuangamiza ndoto na malengo yako.

Kwa mfano mtu akakushawishi uingie kwenye biashara ya dawa za kulevya, je unafikiri utaweza kweli kupata manufaa ya uhakika? Unaweza kukamatwa na maisha yako yakaishia gerezani.

Huu ni mfano wa mipango mibaya ambayo watu wanapaswa kutokusita kusema hapa; kumbuka hakuna mkato kwenye mafanikio.

2. Kusema Hapana Hukufanya Kuonekana Mwenye Msimamo

Tutatambua vipi msimamo wako ikiwa wewe unakubali kila kitu? Ni muhimu kusema hapana ili watu watambue kuwa una masimamo fulani ambao hauwezi kuuacha.

Ikiwa kuna jambo au kitu ambacho hukipendi, basi tumia buasara kusema hapa ili watu waheshimu msimamo wako.

Kwa mfano ikiwa wewe hutumii pombe au sigara, basi sema wazi hapa kwa vitu hivi hata kama hutamfurahisha unayempa jibu hilo.

3. Kusema Hapana Hufanya Mawazo Yako Yaheshimike

Watu wataheshimu mawazo yako kama unayabainisha na kuyatetea wazi. Kusema hapana ni njia ya kuonyesha aina ya mawazo uliyonayo.

Tumia hekima na busara kupinga mawazo yale ambayo wewe huyataki; moja kwa moja wale unaowaeleza wataweza kutambua wazi mawazo yako na kuyaheshimu.

4. Kusema Hapana Huokoa Fedha na Muda

Unaposema hapana utaepuka mambo na tabia mbalimbali ambazo zinaweza kukupotezea muda na pesa nyingi.

Ni muhimu kusema hapana kwa maswala kama vile pombe, uzinzi, matumizi mabaya mitandao ya kijamii au uzururaji.

5. Kusema Hapana Hukuwezesha Kufikia Ndoto Yako

Ili tuweze kufikia ndoto zetu tunahitaji kuepuka mambo mbalimbali yasiyoendana na ndoto au maono yetu.

Ka njia ya kusema hapana unaweza kuondoa mambo yote ambayo kwa namna moja au nyingine hayakuwezeshi kutimiza ndoto au maono yako.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply