Kilimo Cha Matango Tanzania

Kilimo cha Matango ni Kilimo Kizuri sana kwa Tanzania kwasababu matango ni zao linalopendelea hali ya hewa ya joto na hustawi vyema kati ya nyuzi joto 18°C hadi 35°C

Udongo Mzuri Kwa Kilimo Cha Matango

Hustawi vizuri katika udongo tifutifu wenye rutuba usiotuamisha maji.

Maandalizi Ya shamba La Matango

Lima shamba kwa trekta, kwa ng’ombe ama kwa jembe la mkono kwa kina cha sentimita 30 hadi 45 na weka matuta ya mwinuko yenye upana wa mita 1 hadi 1.5 kutoka kati ya tuta na tuta

Jinsi Ya Kupanda Matango

Zipo aina mbili za upandaji wa matango

  1. kupanda mbegu moja kwa moja na
  2. kupanda mbegu katika trei na kuhamisha baada ya siku 8 hadi 10.

Njia ya kupanda mbegu moja kwa moja ni rahisi lakini ile ya kupanda katika trei ni bora zaidi kwani shamba hujaa vizuri katika nafasi na hukua haraka na kuzaa mavuno mengi.

Pima mashimo ya kupandia katika umbali wa sentimita 20 hadi 25 kutoka shina hadi shina mstari mmoja kwa tuta na sentimita 40 katika mfumo wa zig-zag pande zote mbili za tuta na kupanda.

Mbolea kianzio iwekwe katika kila shimo na kupanda endapo miche kutoka katika trei itatumika Hakikisha shamba lina unyevu wa kutosha kabla ya kupanda

Jinsi Ya Kupalilia Matango 

Palilia shamba mara kwa mara ili kuhakikisha shamba halina magugu Magugu hudhibitiwa kwa palizi ya jembe, kung’oa kwa mkono ama matumizi ya viuagugu.

Njia nyingine ni matumizi ya plastiki maalum kuzuia magugu yaani ‘plastic mulch’.

Jinsi Ya Kuweka Mbolea 

Tumia mbolea ya DAP wakati wa kupanda na kisha tumia NPK yenye uwiano mmoja kama, 18:18:18, 17:17:17 ama 16:16:16 baada ya wiki tatu toka Usegekaji.

Tumia nguzo za unene wa inchi 2 na kamba ili kuinua mimea na matunda yasiguse ardhi na kuoza.

Uchavushaji wa zao La Matango

Hii ni muhimu sana kuzingatiwa kwani tango huchavushwa kwa wadudu na si upepo. Bila wadudu kama nyuki uzalishaji huathrika sana.

Ni muhimu kupanda mazao kama alizeti na maua mbali mbali yanayopendwa na wadudu wachavushaji ili kuhakikisha uwepo wa wadudu hao shambani.

Aidha inapo-lazimu ni vema kuweka mizinga kadhaa ya nyuki katika shamba la tango

Matumizi ya viuatilifu Katika udhibiti wa wadudu na magonjwa matumizi ya viuatilifu yafanyike kwa maelekezo ya wataalam kubaini tatizo na kiuatilifu hitajika na namna ya matumizi yake

Mavuno Ya zao La Matango 

Mavuno huanza baada ya siku 40 hadi 45 kutegemea na aina pamoja na hali ya hewa.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply