Kilimo Cha Bustani Tanzania

Kilimo cha Bustani Tanzania ni kilimo kizuri sana na ili kupata bustani iliyobora wewe kama mkulima ni lazima uwe muangalifu wakati wa kupanda bustani yako.

Mambo ya kuzingatia kwenye kilimo cha bustani

1. Mwinuko

Eneo lisiwe kwenye mwinuko mkali kwa sababu sehemu kama hizo zinaweza kusababisha mmomonyoko wa udongo. Endapo sehemu itakuwa ya mwinuko tengeneza matungazi (terrace) ili kuzuia mmomonyoko.

2. Udongo

Udongo unaofaa ni wenye rutuba, mboji nyingi na unaopitisha maji kwa kirahisi. Vilevile usiwe na historia ya magonjwa na wadudu waharibifu.

3. Chanzo cha Maji

Eneo la bustani liwe karibu na maji ya kudumu. Maji yasiwe na chumvi nyingi kwani huathiri ukuaji wa mimea.

4. Kitalu

Kitalu kisiwekwe mahali palipo na kivuli kingi kwa kuwa husababisha mimea kuwa dhaifu.

Kuzuia Upepo Mkali

Eneo la bustani lipandwe miti mipakani ili kuzuia upepo mkali. Upepo mkali huharibu mimea kwa kuvunja vunja majani na matawi na husafirisha vimelea vya magonjwa na wadudu.

Pia hufanya udongo wa juu kukauka haraka na kuleta mmomonyoko.

Jinsi Ya Kutayarisha Matuta Ya Bustani

Ni muhimu udongo utifuliwe vizuri. Mabonge makubwa yavunjwe vunjwe ili Kurahisisha upitaji wa maji na hewa katika udongo.

Matuta huinuliwa kidogo toka usawa wa ardhi ili kuzuia maji yasituame. Matuta haya yasitumike wakati wa kiangazi.

Wakati wa kiangazi tengeneza matuta yaliyo didimia kidogo.

Jinsi Ya Kumwagilia Maji Kwenye Bustani

Hakikisha udongo una unyevu wa kutosha kwa kumwagilia siku moja kabla ya kuotesha mbegu. Pia baada ya kupanda mwagilia kitalu au shamba maji ya kutosha. Maji mengi husababisha mbegu au miche kuoza.

Jinsi Ya Kupanda Bustani

Kina cha kupanda kitategemea ukubwa wa mbegu. Mbegu ndogo hupandwa katika kina kifupi zaidi kuliko mbegu kubwa.

Upandaji wa baadhi ya mbegu unaweza kufanyika kila wiki ili kuweza kupata mboga mfululizo.

Jinsi Ya Kuotesha Mbegu Kwenye Kitalu

Baadhi ya mbegu za mboga huoteshwa kwanza kwenye kitalu na baadaye miche huhamishiwa shambani. Mbegu hizini kama vile za bilinganya, kabichi, nyanya, pilipili hoho na vitunguu.

Kitalu kwa ajili ya kuotesha mbegu hakina budi kitayarishwe wiki moj a kabla ya kusia mbegu. Wakati wa kutayarisha kitalu, ardhi ikatuliwe katika kina cha kutosha sentimita 30 kwenda chini.

Katika kuongeza rutuba ya udongo tumia mbolea za asili kama vile samadi, takataka na mbolea vunde zilizooza vizuri ziwekwe kabla ya kusia mbegu.

Jinsi Ya Kutumia Mbegu Bora

Tumia mbegu bora zilizohifadhiwa kwenye dawa. Mbegu bora ni zile ambazo zimekomaa na kukauka vizuri, hazikushambuliwa na wadudu wala magonjwa na ambazo zina uwezo wa kuota vizuri.

inashauriwa kutumia mbegu zilizothibitishwa kitaalamu.

Jinsi Ya Kuweka Kivuli Kwenye Bustani Yako

Utandazaji wa majani makavu na uwekaj i wa kivuli ni muhimu ili kuzuia jua linaloweza kunyausha miche pia matandazo pia husaidia kuhifadhi unyevu, joto la udongo na hupunguza palizi ya mara kwa mara.

Kivuli kiruhusu mwanga wa kutosha na kiondolewe kidogo kidogo kadiri mimea inavyokua.

Uwekaji wa kivuli ni muhimu ili kuzuia jua kali

Jinsi Kuitayarisha Miche Kabla Ya Kupandikiza

Wiki mbili kabla ya kuihamisha miche toka kitaluni, unashauriwa kupunguza kumwagilia ili kuizoesha iweze kustahimili hali ya sehemu inapohamishiwa.

Mwagilia kitalu siku moja kabla ya kung’oa miche ili kurahisisha ung’oaji na kuepuka kuikata mizizi. Pia shamba kwa ajili ya kuhamishia miche limwagiliwe siku moja kabla ya kupandikiza ili kuloanisha udongo.

Aina za Mbolea na Matumizi Yake

1. Mboji, Samadi na Mbolea Vunde

Mboga hustawi, vizuri sana katika udongo wenye mbolea hizo kwaio ni vema mbolea hizo ziwekwe shambani kabla ya kupanda au kupandikiza.

Kiasi kinachotakiwa ni ndoo moja kwa tuta lenye upana na urefu wa mita moja.

2. Mbolea za Viwandani

Mbolea za viwandani zimegawanyika katika makundi makuu matatu, nayo ni mbolea za chumvichumvi, chokaa na kijivu,

Jinsi Ya Kubadilisha Mazao Kwenye Bustani

Kubadilisha mazao shambani ni utaratibu wa kuachs kupanda mfululizo aina ileile ya zao katika eneo hilo hilo.

iwapo eneo ni kubwa, bustani igawanywe katika sehemn tatu au nne ili kuepuka kupanda mfululizo aina ileile ya zao.

Pia Katika kila sehemu panda aina nyingine ya mazao na ya familia tofauti kila baada ya kuvuna.

Kubadilisha mazao shambani huzuia ongezeko la wadudu na magonjwa yanayoshambulia jamii moja ya zao.

Vilevile huhifadhi rutuba ya udongo na huzuia uotaji wa magugu pia taratibu huu pia humwezesha mkulima kuweka kiasi cha mbolea kinachotakiwa shambani.

Baadhi Ya Mazao Mazuri Ya Bustani

1. Jamii Ya Nyanya
  • Bilinganya
  • Nyanya
  • Pilipili
  • Viazi Mviringo
2. Jamii Ya Matango
  • Matango
  • Maboga
  • Matikiti Maji
3. Mimea Ya Mizizi
  • Karoti
  • Vitunguu

Matumizi Ya Dawa Kwenye Bustani

Ni muhimu kutumia madawa ili kukinga mimea kutokana na athari za wadudu na magonjwa. Hata hivyo madawa yatumike pale inapobidi kwani ni ghali na yana madhara kwa mazingira na watu.

Mambo yafuatayo yanatakiwa kuzingatiwa wakati wa kutumia madawa. Hakikisha unatumia dawa inayoshauriwa na wataalamu.

  1. Soma kwa uangalifu maelezo yanayoambatana na dawa toka kwa watengenezaji, kabla ya kutumia na yasikiukwe. Hii itakusaidia kujua vifaa, kiasi na jinsi ya kutumia. Madawa ni hatari kwa binadamu na wanyama kama yatatumika isivyopasa.
  2. Wakati wa kuchanganya na kunyunyizia dawa, vaa nguonavifaavyakinga. Vifaa hivi ni kofia, glovus, viatu (gumboots), kitambaa cha kufunika mdomo na pua, miwani na ovaroli.
  3. Tumia maji safi kuchanganya dawa.
  4. Epuka kuvuta hewa yenye dawa. Wakati wa kunyunyizia dawa usielekee upepo unakotoka bali elekea upepo unakoenda.
  5. Usile wala kuvuta wakati wa kuchanganya au kunyunyizia dawa.
  6. Baada ya kunyunyizia dawa osha mwili kwa sabuni na maji mengi na safi.
  7. Maji yanayotumika kusafishia bomba yasimwagwe katika maji yaliyotuama au yanayotembea kwani yanaweza kuleta madhara sehemu nyingine. Maji yamwagwe kwenye shimo na kufukiwa.
  8. Nguo na vifaa vingine vilivyotumika zifuliwe mara moja kwa sabuni na maji safi.
  9. Osha vizuri mikono kwa sabuni kabla ya kula, kunywa chochote au kuvuta sigara.
  10. Makopo au chupa zilizokuwa na dawa zisitumike bali ziharibiwe na kufukiwa.
  11. Hifadhi madawa mahali salama na pasipofikiwa na watoto kwa urahisi. Dawa ziachwe katika makasha., chupa au makopo yake zilimokuwemo. Hata siku moja madawa ya mimea yasitumike kwa kutibu binadamu.
  12. Endapo kutakuwepo na matatizo yeyote katika matumizi muone Mtaalamu kwa ushauri.
  13. Iwapo sehemu ya kutolea dawa itaziba, tumia nyasi au kijiti kuzibua. Kamwe usizibue kwa mdomo.

Jinsi Ya Kutumia Mboga Baada Ya Kunyunyizia Dawa

Mboga zisitumike mara baada ya kunyunyizia dawa. Kila dawa ina siku zake za salama, lakini kwa madawa yaliyo mengi ni siku 14 toka kunyunyizia.

Hivyo ni muhimu kusoma maelezo yanayoambatana na dawa. Ikiwa mboga zitatumika kabla ya muda huo huleta madhara kwa mlaji kama vile magonjwa ya kansa.

Vilevile mbegu zilizowekwa dawa zisitumike kwa kula.

Magonjwa Na Wadudu Waharibifu

Ni muhimu kukinga mimea dhidi ya wadudu na magonjwa ili kupata mazao mengi na bora. Zifuatazo ni njia mbalimbali zinazoweza kutumika katika kuzuia magonjwa na wadudu waharibifu.

Udhibiti wa Ugonjwa wa Sango

Njia hii hutumia mbinu zifuatazo;

  • Kupanda mbegu bora;
  • Usafi wa bustani ambao ni pamoja na kuchoma takataka na kuondoa magugu yanayoweza kutunza wadudu na magonjwa.
  • Kuchanganya mazao
  • Kutumia samadi na mboji
  • Kupanda kwa nafasi
  • Kutumia aina ya mbegu zinazovumilia au kustahimili mashambulizi ya magonjwa na wadudu

Udhibiti Wa Kiteknolojia Kwenye Bustani

Kutumia aina mbalimbali za madawa

  • Kutumia mimea inayoua wadudu, kama vile muarobaini, pilipili kali, aina fulani ya maua, marejea, tumbaku, wadudu kama vile walawangi, manyigu na mbawakau.

Vifaa vya Kwenye Bustani

Kwenye kuboresha kilimo cha mboga ni muhimu kuwa na jembe, kamba, reld, uma wa bustani, ndoo ya kumwagilia maji, bomba la kunyunyizia dawa, toroli, panga, kwanja, sepetu, beleshi karai na kadhalika.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply