Ufugaji wa Nguruwe Kibiashara Tanzania

Ufugaji wa nguruwe Tanzania

Ufugaji wa nguruwe ni wa watu wa kada zote, wafugaji wadogo wadogo na hata wakubwa pia ufugaji wa nguruwe huweza kumpatia mfugaji kipato pamoja na chakula kwa familia, na hauhitaji gharama kubwa.

Vitu vya kuzingatia katika ufugaji WA nguruwe

1. Banda la ufugaji wa nguruwe

Nguruwe wanahitaji kuwa na banda lililojengwa kwa vifaa nafuu Unaweza kutumia mchanga na simenti kuweka sakafu, ama ukatumia udongo wa mfinyanzi kwa ajili ya kuweka sakafu.

Ukubwa wa banda unategemeana na idadi ya nguruwe na aina ya ufugaji wa nguruwe unaotaka kufanya. Mita 3 kwa mita 2.5 zitawaweka guruwe 8-10 wanaonenepeshwa kwa soko au nguruwe jike mmoja na nguruwe ndume mmoja.

2. Chakula Cha nguruwe

Katika ufugaji wa nguruwe ulishaji wake ni rahisi kwa kuwa wanakula aina mbalimbali za vyakula kulingana na mazingira wanayofugwa Unaweza kuwalisha kwa kutumia majani laini ya aina mbalimbali na pia hulishwa kwa kutumia masalia ya nafaka (pumba).

Unaweza kuwalisha kwa kutumia mashudu au pumba aina ya Wheat Poland Pia unaweza kuwalisha kwa kutumia mabaki ya jikoni.

3. Kuzaliana kwa nguruwe

Nguruwe hubeba mimba kwa kipindi cha siku 114, ambazo hugawanyika kwa miezi 3, wiki 3 na siku 3 Nguruwe mmoja ana uwezo wa kuzaa watoto 6 hadi 14 kwa mara moja Watoto wa nguruwe (piglets) huanza kula chakula cha kawaida wanapofika umri wa mwezi mmoja na nusu mpaka miezi miwili.

Endapo nguruwe watapata matunzo mazuri, baada ya miezi 8 wanakuwa na uzito kati ya kilo 50-70 na wanaweza kuuzwa.

4. Matunzo ya nguruwe

Katika ufugaji wa nguruwe Baada ya nguruwe kuzaa anatakiwa kupatiwa chakula cha kutosha na cha kutia nguvu ili kupata maziwa ya kutosha kwa ajili ya watoto wake.

Watoto wa nguruwe wachomwe sindano ya madini ya chuma (Iron injection) baada ya siku moja au mbili toka kuzaliwa.

Hii ni muhimu sana vinginevyo wanaweza kufa wote Kata meno (tooth clipping) baada ya miezi mitatu Unaweza kuhasi madume (castration) baada ya miezi miwili.

Magonjwa ya nguruwe

Kuna aina nyingi za magonjwa katika ufugaji wa nguruwe lakini yapo yale yaliyozoeleka ambapo ni lazima kukabiliana nayo ili kuwa na ufugaji wa nguruwe wenye tija.

1. Ugonjwa wa miguu na midomo

Ugonjwa huu huathiri nguruwe sehemu za miguu na midomo Ni ugonjwa ambao hushambulia nguruwe mara kwa mara hasa wasipokuwa na matunzo mazuri Ugonjwa wa miguu na midomo hudhoofisha nguruwe kwa haraka sana ikiwa ni pamoja na kupungua uzito.

Chanjo: Chanjo kwa ajili ya ugonjwa wa midomo na miguu (FMD vaccine) hutolewa kila baada ya mwaka mmoja Hii inasaidia kuwaweka nguruwe wako katika hali nzuri zaidi bila kushambuliwa na magonjwa hayo.

Tiba: Ugonjwa huu hauna tiba halisi Inapotokea nguruwe wakawa wameshambuliwa kinachofanyika ni kutibu magonjwa nyemelezi kwa kutumia antibiotics.

2. Homa ya Nguruwe (Swine fever)

Virusi vinavyosababisha ugonjwa wahoma ya nguruwe huenea kwa haraka sana miongoni mwa makundi ya nguruwe na huua kwa haraka sana lakini hauna madhara kwa binadamu na hauambukizwi kwa binadamu.

Nguruwe walioambukizwa wana shikwa na vindonda ama mapunye kwenye ngozi Pia masikio na ngozi huwa mekundu.

Chanjo: Ugonjwa huu hauna chanjo wala tiba Kinachofanyika mlipuko unapotokea ili kuwa salama ni kuwateketeza nguruwe wote walioathirika na kuanza upya ufugaji wa nguruwe Unaweza kuteketeza nguruwe kwa kuwachoma moto.

Muhimu: Baada ya kuwateketeza nguruwe wagonjwa safisha banda kisha nyunyiza dawa aiana ya Acon au Ectomin na uache banda wazi kwa kipindi cha wiki moja kabla ya kuanza ufugaji wa nguruwe wengine.

3. Ugonjwa wa mapafu (Pneumonia)

Huu ni ugonjwa unaoshambulia sehemu za koo na mapafu ya nguruwe ambapo husababisha kukohoa na kupumua kwa shida.

Ugonjwa huu husababishwa na bacteria (Secondary bacterial), joto kupita kiasi, vumbi na gesi inayotokana na madawa makali.

Tiba: Homa ya mapafu kwa nguruwe inatibika kwa kutumia antibiotics Pamoja na kuwaweka wanyama sehemu safi, isiyo na baridi kali au joto la kupitiliza kiwango.

4. Kimeta (Anthrax)

Huu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria wanaojulikana kama Bacillus anthracis wadudu hawa wanabaki kuwa hai kwa muda mrefu na wanaweza kuwa kwenye udongo wakiwa hai kwa kipindi cha miaka mingi.

Chanjo: Chanja nguruwe wako dhidi ya kimeta kama utakavyoelekezwa na wataalamu wa mifugo walio karibu nawe.

Tiba: Unaweza kutibu nguruwe wako kwa kutumia dawa aina ya Penisilin au Oxytetracycline.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

16 Comments
  1. Nguruwe watoto ni Bei gani kutoka kwa wauzaji wa nguruwe tanzania?

  2. Habari wauzaji, Naombeni mniunganishe kwenye group la ufugaji wa nguruwe Tanzania pamoja na group la wauzaji wa nguruwe Tanzania Mimi pia ni mfugaji

  3. Asanteni Kwa elimu yenu ya Ufugaji wa Nguruwe nimepata mwangaza sana.

  4. Tunashukuru kwa somo la ufugaji. Je nitapata soko la kuaminika la nguruwe Kama nitawazalisha kwa wingi?

  5. Naomba mniunganishe katika group lenu na mimi Nawaza kuanza kufuga Nguruwe ninaishi Mlandizi Mkoani Pwani.

  6. Sisi pia kule kwetu tunafanya ufugaji wa nguruwe ni biashara nzuri sana.

  7. Ama kweli darasa linanoga najikuta naongeza uelewa na natumaini mapaka mwaka huu kuisha nitakuwa mbali sana ama kweli nguruwe ndio habari ya town.

  8. Nashukuru kwa elimu hii ya ufugaji wa nguruwe wa biashara.

Leave a Reply to Lenald Minja Cancel reply