
Vitu vya kukazana na kujitahidi kuviacha kabisa ili uweze kufanikiwa kwenye maisha Tanzania ni muhimu kuvifahamu mapema.
1. Jitahidi Kuacha Kutoa Visingizio
Acha kulaumu na kulalamikia watu wengine kwa kutokupata kile unachokihitaji. Acha kusingizia serekali na jamii kuwa ndiyo kikwazo cha wewe kufikia mafanikio yako.
Kumbuka hakuna mtu aliyefanikiwa sana duniani kwa kusaidiwa na serikali au mtu fulani katika jamii ukiwepo msaada basi utumie tu kama ngazi.
Watu waliofanikiwa hawalalamiki bali wanafanya kazi kwa bidii kufikia malengo yao.
2. Jitahidi Kuacha Kutazama Mapungufu
Umejijengea dhamiri ya kutofanya chochote kwa kuwa wewe unaona tu matatizo. Kwa hakika katika ulimwengu huu kila kitu kina pande mbili; unachotakiwa kufanya ni kuyaona matatizo kwa jicho la mafanikio.
Badili mtazamao wako sasa epuka kuona tu matatizo na mapungufu ili uweze kufanya mambo yenye tija kwa ajili ya mafanikio yako.
3. Jitahidi Kuacha Kuogopa Kushindwa
Mara nyingi napenda kuwashauri watu kuwa ni bora kujaribu ukashindwa kuliko kushindwa hata kujaribu. Umekuwa haufanyi kitu chochote kwa kigezo kuwa unaogopa kushindwa hakika hotofanikiwa kwani maisha yako yatamalizika wakati hujafanya chochote.
Je ulishwahi kufikiri kila mtu ulimwenguni angewaza kama wewe? Dunia hii isingekuwa na ugunduzi wala maendeleo yoyote.
Mwanasayansi Thomas Edison alijaribu mara 1,000 kutengeneza balbu ya umeme hadi alipofanikiwa. Je kwanini wewe hujajaribu hata mara moja? Anza kufanya leo na utaona matokeo yake.
4. Jitahidi Kuacha Kutafuta Njia Rahisi
Wahenga walisema rahisi ni gharama; pia wakesema rahisi inaumiza. Fahamu kuwa hakuna kitu kizuri kinachopatikana kwa urahisi.
Jiulize ni kwa nini madini ya thamani hupatikana chini sana ardhini; baada ya swali hili utagundua kuwa kufikia mafanikio ni kupambana na changamoto.
Fanya kazi kwa bidii, tumia nguvu, juhudi na marifa yako yote ili uweze kufikia malengo yako ya maisha. Acha uvivu tesa mwili na akili yako kwa muda, kwani utaona matokeo mazuri.
5. Jitahidi Kuacha Kujipiga Mwenyewe
Kama hapendi kujipiga au kuumiza mwili wako wa damu na nyama kwanini unaruhusu kupiga au kuumiza akili na fikra zako?
Acha kuwaza mawazo yanayoumiza akili na fikra zako; yaliyopita yamepita, yasahau ujenge maisha mapya. Hakikisha huumizi fikra na akili zako kwani zinahitajika sana katika kufanikiwa kwako.
6. Jitahidi Kuacha Kutokuwa na Shukrani
Jifunze kusukuru na kuridhika kwa vitu na hali uliyonayo. Inawezekana kuna wengine wanatamani hata wawe na uwezo wa kuwa wazima kiafya lakini hawawezi.
Simaanishi uridhike na matatizo, la hasha, bali ujifunze kutambua unapopata mafanikio fulani; kwani hili litakuhamasisha kusonga mbele zaidi. Nimeshuhudia watu ambao wana mafaniko mengi tu lakini bado wanahangaika na kunung’unika kama vile hawana hitu. Hivyo badili mtazamo wako leo.
Ni wazi kuwa, ukiwa na shukurani pia utajifunza kuridhika.
7. Jitahidi Kuacha Kabisa Ubinafsi
Inawezekana unawaza sana kuhusu maisha yako na mahitaji yako, tena unafikri kuvipata hivyo ndiko kufanikiwa. Hakia kufanikiwa halisi ni kuweza kuwasaidia na kuwafikia wengine.
Pia kutumia mahitaji au matatizo ya wengine kama fursa ni njia bora zaidi ya kuhimiza mafanikio yako.
8. Jitahidi Kuacha Kuvurugwa
Kuvurungwa? Ndiyo, kuvurugwa kunaweza kukutoa katika njia sahihi ya mafaniko yako. Unataka kuandika kitabu lakini… unataka kusoma lakini… unataka kuanzisha biashara lakini… unajikuta kuna mtu au kitu kinakuingilia.
Usiruhusu mtu au vitu kama vile mitandao ya kijamii kukutoa katika kufanya kile unachotaka kukifanya; jitenge navyo kisha fanyia kazi malengo yako.
9. Jitahidi Kuacha Kuishi Bila Malengo
Watu wengi hawana malengo wala hawafahamu maana na umuhimu wa malengo katika maisha yao. Malengo hukuwezesha kuona kituo au fikio fulani la baadaye katika maisha yako. Jiulize leo una malengo?
Je unafanya jitihada kuyafikia? Kama jibu ni hapana, hakika itakuwa ni vigumu sana kwa wewe kufanikiwa. Badili fikra zako sasa, jiwekee malengo na uyafuate
10. Jitahidi Kuacha Kukata Tamaa Mapema
Ni kweli kuwa changamoto zipo kila siku kwenye maisha yetu, lakini hatutakiwi tuziruhusu zitukatishe tamaa.
Inawezekana umekaribia kabisa kufika kwenye mafanikio lakini kutokana na upepo na mawimbi mengi katika njia yako unaamua kuacha na kurudi nyuma.
Nilikuwa natamani sana kufahamu ni mbinu zipi nitazifanya Ili niweze kufanikiwa Asanteni sana.
Asante sana Abdallah kwa comment yako na mimi nimefurahi kusikia hivyo.