Magonjwa yanayoshambulia nguruwe yana tiba pia ni mengi kama ilivyo kwa wanyama wengine yanavyotokea lakini kuna magonjwa katika ufugaji wa nguruwe lazima uyajue pamoja na tiba zake kwakua ndio yanayo jitokeza mara kwa mara
1. Ugonjwa wa miguu na midomo kwa nguruwe
Huu ni moja ya magonjwa ya nguruwe Ugonjwa huu huathiri midomo na miguu ya nguruwe Ni ugonjwa ambao hushambulia nguruwe mara kwa mara hasa wasipokuwa na matunzo mazuri Ugonjwa wa miguu na midomo, hudhoofisha nguruwe kwa haraka sana, ikiwa ni pamoja na kupungua uzito.
Chanjo: Chanjo yake huitwa FMD VACCINATION nautolewa kila baada ya mwaka mmoja
Dalili: dalili zake miguu na midomo ya nguruwe inabadilika na pia nguruwe anadhoofika
Tiba: Ugonjwa huu hauna tiba halisi Inapotokea nguruwe wakawa wameshambuliwa kinachofanyika ni kutibu magonjwa nyemelezi kwa kutumia antibiotics.
2. Ugonjwa WA homa ya nguruwe
Ugonjwa huu unasambaa kwa kasi kama mmoja akiambukizwa wengine pia wataambukizwa na kufa
Dalili: nguruwe anakua na vidonda na vitu kama vibarango mwili mzima pia mdomo na masikio yanabadilika rangi nakua mekundu.
Chanjo: Ugonjwa huu hauna chanjo wala tiba. Kinachofanyika mlipuko unapotokea ili kuwa salama ni kuwateketeza nguruwe wote walioathirika na kuanza upya. Unaweza kuteketeza kwa kuwachoma moto.
Muhimu: Baada ya kuwateketeza nguruwe wagonjwa, safisha banda kisha nyunyiza dawa aiana ya Acon au Ectomin, na uache banda wazi kwa kipindi cha wiki moja kabla ya kuweka nguruwe wengine kwa kua huu ni viral disease
3. Ugonjwa wa mapafu kwa nguruwe
Huu ni moja ya magonjwa ya nguruwe ambayo Ushambulia sehemu za koo na mapafu ya nguruwe, Ugonjwa huu husababishwa na bacteria (Secondary bacterial), joto kupita kiasi, vumbi na gesi inayotokana na madawa makali.
Dalili: nguruwe hukooa na kupumua kwa shida sana
Tiba: Homa ya mapafu kwa nguruwe inatibika kwa kutumia antibiotics Pamoja na kuwaweka wanyama sehemu safi, isiyo na baridi kali au joto la kupitiliza kiwango.
4. Ugonjwa WA kimeta
Huu ni moja ya magonjwa ya nguruwe unaosababishwa na bakteria wanaojulikana kama Bacillus anthracis, wadudu hawa wanabaki kuwa hai kwa muda mrefu na wanaweza kuwa kwenye udongo wakiwa hai kwa kipindi cha miaka mingi
Tiba: Unaweza kutibu nguruwe wako kwa kutumia dawa aina ya Penisilin au Oxytetracycline.
Asante kwa elimu hii ya ufugaji. Mimi ni mfugaji mpya ndio naanza niko arusha.
Napenda taarifa mbalimbali na ushauri juu ya ufugaji wa nguruwe.
Karibu sana na endelea kusoma post zetu za ufugaji nazani Utapata Taarifa nyingi sana kuhusiana na ufugaji wa tanzania.
Asante kwa mafunzo ya Ufugaji ila mimi nguruwe wangu anatapika na hasikii kula kitu chochote jamani na amedhoofika nifanyeje na huu ni ugonjwa gani wa nguruwe?
Kwenye Ufugaji wa Nguruwe Yapo Magonjwa Yana Wasumbua sana Hivyo Ni Vyema Ukimuona Daktari wa Mifugo Kwa Haraka ili Aweze Kuwaangalia na kisha Akupatie Ushauri.
Asante kwa maelezo yako siku zote dalili za magonjwa ya nguruwe zinatia hofu sana.
Yanatia hofu sana ndio maana ni vizuri kujifunza jinsi ya kufahamu dalili za magonjwa ya nguruwe mapema zaidi.