Kilimo Bora Cha Mkonge Tanzania

Kilimo cha Mkonge ni moja kati Kilimo cha biashara Tanzania Asili ya zao hili ni Mexico na baadae likasambaa katika nchi nyingine nyingi ikiwemo Tanzania

Na kwa mara ya kwanza lilitambushwa katika nchi za kitropikia na subtropikia India, Tanzania, Brazil, Kenya south Africa, Angola, Mozambique, Morocco, Uganda, Zimbabwe na Mauritius na katani ni zao ambalo hutumika sana kutengenezea bidhaa nyingi.

Hali ya hewa ya kilimo cha mkonge

JOTO; Katani hukua vizuri katika maeneo ya kisubtropikia, yaani hukua vizuri kwenye maeneo ya joto yenye joto kati ya 10-32 oC na joto ya juu zaidi inakua 30 hadi 40oC na joto ya hali ya chini zaidi ni 5oC.

MVUA; Pia mvua huchukua nafasi muhimu katika kilimo cha katani zao hili  huzaa vyema zaidi katika maeneo yenye mvua 500mm na zaidi kwa mwaka na wastani wa mvua 600mm hadi 1500mm na pia huweza kukua kwenye maeneo yenye mvua chini ya hapo.

UDONGO; Zao la katani halibagui sana udongo lakini hukua vyema kweye maeneo ambayo yana unyevu wa kutosha na aina nyingi za udongo isipo kua udongo mfinyanzi na pH 4.0 hadi 6.0 ni muhimu.

MBEGU Katani hupandwa kwa kutumia bulbils na suckers.

Suckers; ni vile ambavyo vinakua karibu na mmea na utokana na matokezi (buds) na vinaweza kuchukuliwa na kupandwa moja kwa moja shambani

Bulbils; Pale katani inapokua huzaa maua katika mlingoti wake, hivi huchukuliwa na kupandwa katika kitalu na watu wengi hupenda kuaanda hivi kwa kua hua na sifa kamili kama ya mmea ambao ni mzazi.

Jinsi ya kuandaa shamba la mkonge

Mfumo unao hitajika ni ule wa mistari miwili yaani double rows. Hivyo andaa shamba kwa kulipalilia vizuri na kuondoa taka zote.

Jinsi ya kupanda zao la mkonge

Mkonge lazima upandwe kweye kitalu kwanza vinapandwa  10cm x 10cm na hukaa kwenye kitalu kwa muda wa miezi 6 na baada ya hapo huamishiwa tena kwenye kitalu kikubwa ambapo hupandwa kwa 30cm x 30cm.

Na baada ya miezi 12 hadi 18 mimea wa mkonge huwa tayari sasa kwa kupandwa katika shamba kubwa na nafasi kati ya mistari hua  ni 1 hadi 1.5 m na 4 m na kina cha kupanda mmea hua ni 3cm  katika kuhamishia shambani mizizi midogo  pembeni ya mmea hukatwa  na majani ya chini yanaweza kuondolewa.

Mbolea katika kilimo cha katani

Katani hua haiitaji sana mbolea kwakua hua na urafiki na mazingira pale inapo pandwa kwenye eneo jipya lakini inapo pandwa kwenye eneo ambalo limekwishatumika mbolea huitajika na unaweza kutumia UREA, lime ammonium nitrate (LAN) na superphosphate.

Umwagiliaji wa zao la katani

Kilimo cha katani hakihitaji umwagiliaji kwa kua huhimili ukame japo kua katika kuprocess maji hutumika sana.

Upaliliaji wa kilimo Cha mkonge

Kupalilia ni muhimu sana ndani ya miaka miwili ya mwanzo yaani miaka 2 hadi 3 ni vyema sana kupalilia baada ya kuamishia katika shamba kubwa unaweza kutumia jembe la mkono au hata kemikali pia unaweza kuacha magugu kukua wakati wa mvua na uka palilia wakati mvua zimeisha.

Magonjwa na wadudu wa zao la katani

Wadudu

  • Weevil wa katani
  • nguruwe
  • nyani na sokwe

Unaweza kuuwa wadudu kwa kutumia viua dudu ambavyo vimesajiliwa na  kwakulinda shamba ili wanyama kama nyani wasishambulie shamba

Magonjwa

  • Madoa ya majani
  • kuoza kwa mringoti

Unaweza kuzuia kwa kuweka mbolea ambazo zina calcium na kwa kuweka shamba safi na pia tumia dawa  za kemikali

Uvunaji wa zao la mkonge

Uvunaji wa zao la mkonge inategemea na eneo, kiasi cha mvua, udongo na hali ya hewa pia lakini kwa kawaida katani huvunwa kwa mara ya kwanza kati ya miaka 3 hadi 4 baada ya kupanda.

Mimea hua na majani 120 hadi 125  ambayo hua na urefu wa 60 cm unatakiwa kuvuna majani ambayo tu yapo tayari.

Majani hua tayari pale rangi inapo badilika kutoka brown iliyo koza hadi kua brown iliyo pauka na majani huvuna kwa interval kwa maana hiyo unaweza kuvuna majani 25 kwa kila mmea kwa mwaka.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

6 Comments
  1. Nimefurahi sana kukutana na platform kama hii inayohusu kilimo kwani kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu.

    Nawaunga mkono na naaidi nitatoa ushirikiano hata kwa kufanya sharing kwa media nyingine ikiwemo mitandao ya kijamii.

  2. Huku kwetu pia wanafanya sana kilimo hiki cha mkonge.

  3. Huwa navutiwa sana na zao hili la mkonge natamani siku na mimi nilime hiki kilimo cha mkonge.

Leave a reply