
Biashara ya kutengeneza juice ya miwa ina faida hivyo imekuwa maarufu sana katika mikoa mbalimbali hapa Tanzania. Hii inatokana na kinywaji cha juice ya miwa kuwa na faida nyingi katika mwili wa binadamu.
Faida ya juice ya miwa mwilini na kwenye biashara
- Juice ya miwa inasaidia ni kusafisha mkojo, figo na kutibu homa ya manjano.
- Juce ya miwa ni kiburudisho ambacho hukata Kiu hasa wakati wa joto.
- Pia miwa ni jamii ya tunda lenye alkali hivyo lina uwezo wa kupambana na saratani hasa ile ya kibofu cha mkojo na saratani ya maziwa.
- Sukari halisia ya miwa ni nzuri kwa mwili kwani ina virutubisho na madini kwa wingi.
- Miwa ina faida nyingi kiafya Juice ya miwa inafahamika na wataalamu wa afya kwa kuwa na uwezo wa kuupa mwili nguvu kwa sababu ya glucose iliyopo. Kijiko kimoja cha juisi ya miwa kina kalori 11.
- Madini halisi na vitamin zinazopatikana katika sukari ni kama phosphorus, calcium, madini ya chuma na potassium.
- Miwa ina upekee wake kwani ina uwezo wa kuongeza maji mwilini, inaupooza mwili na kuupa nguvu.
- Biashara ya juisi ya miwa ni moja kati ya biashara ndogo inayoweza kuanza na mtaji mdogo lakini ikakuletea faida kubwa kama mjasiriamali kulingana na uhitaji wake.
Mambo ya kuzingatia wakati wa kuanzisha biashara ya juice ya miwa
- Mashine ya kukamua miwa – TZS 300,000 – 400,000
- Glasi nzuri za ujazo tofauti – TZS 20,000
- Chujio – TZS 5,000
- Beseni – TZS 8,000
- Ndoo 2 – TZS 5,000
- Jaba kubwa la uchafu – TZS 12,000
- Mtaji wa kununua miwa –TZS 50,000
- Tolori la kusafirisha – TZS 60,000
- Vifaa vingine – TZS 40,000
Jumla ya mtaji wa kuanzisha biashara ya juice ya miwa ni TZS 640,000
Muwa mmoja unaweza ukatengeneza lita 4 za juisi na muwa mmoja unaweza ukaununua kwa TZS 300 kwa bei ya jumla. Lita moja ya juice ya miwa utauza kwa bei ya TZS 1,000 hivyo kwa muwa mmoja unatengeneza TZS 4,000
Mjasiriamali anaweza akaongeza ubunifu kwa kuongeza tangawizi au limao katika juisi yake ya miwa ili kuongeza ladha. Biashara hii ni nzuri hasa inapofanyika sehemu yenye mzunguko wa watu wengi kama stendi ya mabasi, na kwenye masoko
Changamoto za biashara ya juice ya miwa
- Changamoto zinazo wakabili wauzaji wa juice ya miwa ni upatikaji wa bidhaa hiyo kwa msimu
- Baadhi ya watu kutoamini maji wanayotumia wauzaji katika kutengenezea juisi kama ni salama kwa afya zao.
- Serikali imepiga marufuku vinywaji visivyo pimwa na TBS hivyo wakati mwingine ni usumbufu kwa mjasiriamali mdogo wa biashara ya juisi ya miwa.
- Wajasiliamali wa biashara hii wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu wa mazingira bora ya kufanyia kazi zao Mfano uwepo wa wadudu kama nzi na nyuki mahali zinapofanyika biashara ya uuzaji wa juice ya miwa.
Asante kwa Elimu Hii ya Ujasiriamali Pia Nimefurahi sana kupata taarifa kuhusu biashara ya juisi ya miwa.
Hata mimi pia Nimefurahi sana Kuona Umepata Maarifa ya ujasiriamali wa biashara ya juice ya miwa.
Asante kwa elimu hii ya biashara ya juice ya miwa hivi karibuni nitaanza kujifunza jinsi ya kukamua miwa.
Usiogope Kuanza Kujifunza na Naamini Lazima Utafanikiwa Kwenye Hii Biashara Ya Juice ya miwa.
Nimefurahi kuona Hii post yako Asante sana na Pia na naomba uzidi kutujulisha faida za biashara mbalimbali.
Na mimi nimefurahi Pia na Endelea Kutembelea ili Uweze Kupata Maelezo Ya Faida za Biashara za Tanzania.
Nimependa na Nimejifunza Vizuri Biashara ya Juice Miwa Bado Najipanga ipo Siku Najua Nitaanza Kuifanya.
Usiogope Kuanza na Najua Lazima Utafanikiwa Kwasababu Hata Wengine Walikuwa wanaogopa Biashara ya Juice ila Wakaanza na Wakafanikiwa.
Habari biashara ya juice ya miwa naipenda kweli.
Jitahidi uianze mimi naamini kama ukiifanya vizuri biashara ya miwa utapata faida.
Tatizo kwangu ni mashine za kukamua juice hapa najichanga siku ikifika tu naanza hii biashara.
Nakuombea pesa itimie ili na wewe uanze biashara ya juice ya miwa na ufike mbali.
Nashukuru sana kwa kupata elimu nzuri ya biashara ya uuzaji wa juice ya miwa
Asante sana Marko kwa comment yako na mimi nimefurahi kusikia hivyo.
Siku yoyote nikinunua tu mashine ya juice ya miwa basi nitaanza biashara siku hiyo hiyo.
Asante sana Godie kwa comment yako na mimi nakuombea kwa Mungu akusaidie ufanikishe.