Biashara 12 Ambazo Haziitaji Kabisa Mtaji Tanzania

Biashara za mtaji mdogo wengi huamini kuwa lazima uwe na fedha ndio uanzishe biashara na ndio sababu yao kuu ya kukaa bila kujishughulisha

Ukweli ni kwamba mtaji ni moja ya kitu muhimu sana katika kuanzisha biashara lakini kuna aina ya Biashara Ndogondogo unazoweza kuanzisha na kukupelekea kupata faida kubwa sana.

Kama mfanyabiashara unaweza kutoka kwa kishindo sana kwa kuanza ukiwa huna kitu na kufanya kazi kwa juhudi sana ukiwa upande wa huduma (services) na kufanikiwa kutengeneza faida kubwa na kutokea hapo na kuanza kufikiria kuanza kukodi ofisi yako na kuajiri watu wengine

ingawa ni rahisi kutoka ukiwa upande wa huduma lakini inahitaji ujuzi au weledi ili uweze fika kilele cha mafanikio hapa simaanishi lazima uwe umesoma chuo kikuu maana ujuzi au utaalamu wa jambo halihusiani na degree ya chuo kikuu.

Unaweza pata ujuzi kwa kuhudhuria semina mbalimbali, workshop mbalimbali au kufundishwa na mtu wenye ujuzi husika na baada ya kupata ujuzi kuanza fanyia kazi katika maisha yako ya kawaida kila siku na kuwa bora kwa upande huo.

Nimekuandikia biashara 12 ambazo haziitaji mtaji kabisa au mtaji kidogo sana. Hizi ni aina ya biashara ambazo unaweza kuzifanya kwa muda mrefu na kuona matunda yake na nyingine nimeshuhudia watu wakifanya na kufanikiwa.

Kama kweli una shauku ya kuanzisha biashara soma kwa umakini sana na kuona je ni wapi pa kuanzia ili uweze timiza lengo lako la maisha

Biashara ambazo haziitaji mtaji mkubwa

1. Huduma za kuandika mawazo ya biashara kama ilivyo kwa tafiti za uchanganuzi yakinifu (hali halisi ya biashara) wajasiriamali wengi huwa wanaepuka kufanya kazi hii ngumu ya kuandika mawazo ya biashara (business plan) yao

Ukweli ni kuwa wajasiriamali wengi hawajui hata kuandika business plan katika uwezo wa kuwashawishi wawekezaji kuja kuwekeza na huwa hawawekezi muda wa kutosha kujifunza kwa hilo Kama unaweza timiza hitaji hili biashara ipo mikononi kwako.

2. Mshauri wa mambo ya biashara kama Wewe ni mzoefu wa ujasiriamali au mmliki wa biashara au Unajua nini kinahitajika ili uanzishe biashara, kujenga biashara, kuongoza biashara na kukua hapo Sasa unaweza kuanza kazi ya ushauri wa biashara pia Unaweza kusaidia kampuni au biashara mbalimbali kutoka chini ya uvungu na kwa kutoa ushauri na maelekezo muhimu. Unaweza pia kuwasaidia watu walioajiriwa kuanza kutoka kwenye ajira na kuingia kwa ujasiriamali kwa malipo.

3. Huduma za kuandaa vitabu vya mahesabu ikiwa Wewe ni mzuri katika kuandaa vitabu vya uhasibu vya kampuni au biashara mbalimbali unaweza weka ulingano kwa vitabu kwa vya uhasibu Sasa hamna kitu kinaweza kukuzuia wewe kuanza huduma za kuandaa vitabu vya mahesabu anza sasa.

4. Kutoa huduma ya kuandaa nakuendesha matukio (Event management) kampuni nyingi kila mara huwa na matukio mbalimbali mfano semina, siku ya familia, sherehe mbalimbali mara nyingi kampuni kama kampuni haiwezi kufanikisha kwa ufanisi uandaaji wa matukio haya na hivi ndivyo ilivyo kutokana na wafanyakazi wao kuwa na majukumu husika tofauti na kuandaa matukio ya kampuni na kuyasimamia

Hivyo ili kuwa na ufanisi hapa inabidi kampuni zikodi watu wenye ujuzi wa kuandaa shughuli husika kwa uhakika kama una ujuzi na uzoefu wa kuandaa shughuli kama hizo mwanzo mpaka mwisho uwanja ni wako. Mfano kuna matukio kama siku ya familia, semina kwa wafanyakazi, maonyesho ya biashara ndani na je ya nchi kwa kampuni husika

5. Kuanzisha tovuti ya huduma mbalimbali Kwa afrika swala la watu kunufaika na tovuti ndio kwanza ipo steji za mwanzoni Unaweza anzisha tovuti na kutoa huduma ya taarifa kwa watu wanaotafuta baada kuwa na mmiminiko wa watu wengi wanaotembelea tovuti yako unaweza sasa ongea na kampuni kadhaa ili kutangaza na wewe na ukaanza kutengeneza fedha za kutosha.

Kama hujui jinsi ya kutengeneza tovuti usijali kuna tovuti za bure kabisa ambazo zimetengenezwa tayari kinachohitajika ni wewe kujaza fomu zao na ndani ya dakika moja unakuwa na wewe tovuti yako.

6. Mshauri wa masoko mfano wewe unaweza kuwaonesha wafanyabiashara njia ya gharama ndogo ya kuongeza wateja wake kuanzia aslimia 30% -70% au zaidi Pia Unaweza kujiweka wewe mwenyewe kama mshauri wa masoko kwa wamiliki wa biashara ndogo ndogo na kati hata kubwa na kuwafundisha jinsi ya kuteka na kuwavuta wateja na kuongeza mauzo ya bidhaa kwa ada Fulani kutokana huduma yako husika unayoitoa.

7. Mtafasiri wa maandiko mbalimbali kwenda lugha ya wazawa Kampuni nyingi za nje zinazokuja hapa nchini huwa wanahitaji kutafsiri taarifa zao kwenda lugha ya wazawa mfano taarifa za mradi Fulani, tovuti zao, pia kama ni kampuni ya vitabu mwandishi mmiliki angependa ili auze kwa wazawa inabidi atafasiri kwenda lugha ya wazawa.

8. Kutafiti fursa mpya za biashara kuna watu wengi ambao walianza kutoa huduma ya kutafiti fursa mpya na wanafanya vyema kwenye hii biashara. Wanachofanya kutupia jicho kwa mambo yajayo kama mwelekeo, mahitaji au fursa za biashara na kuandaa mipango kuhusiana hilo na kuuza hilo wazo kwa makampuni makubwa.

Wakati mwingine wanakuja na mawazo ya bidhaa na mawazo ya biashara yenye soko moja kwa moja kubwa la kutosha na kuuza hayo mawazo kwa makampuni kwa ajili ya kuayaendeleza Kama kazi hii unaipenda unaweza anza kutoa hudumu kutafiti fursa mpya za biashara

9. Kutoa huduma za ku-print Biashara hii inafahamika sana na wengi lakini bado inalipa sana. Unaweza kuanza kutoa huduma ya ku-print business banner, sposters card, viperushi, flyers, catalogues kwa biashara ndogo na za kati.

10. Kutoa huduma za kuajiri Siku hizi kazi za managementi za rasilimali watu kwa kampuni nyingi hutolewa na tenda kwa kampuni za nje ya kampuni husika kufanya hiyo kazi ili kuongeza ufanisi kwa kampuni husika na hivyo kupelekea kampuni husika kuweka umakini wake wa kutimiza lengo lake mahususi Kama una uelewa na ujuzi wa kutosha wa kushughulika na maswala ya rasiliamali watu uwanja ni wako kwa sasa hapa Tanzania kujisajili kuwa wakala wa kuajiri ni bure unatakiwa uende pale wizara ya ajira na vijana kujisajili.

11. Mshauri wa mitandao ya kijamii (social media consultancy) Kwa hii dunia mitandao ya kijamii imechukua asilimia kubwa sana. Je wewe unajua jinsi ya kutengeneza connection kwa mitandao ya kijamii Unajua jinsi ya kuboresha na kuelimisha umma juu ya chapa (brand) za makampuni ndani ya mitandao ya kijamii kama facebook, twitter na linkedin Basi unaweza kuwa mashauri wa mitandao ya kijamii na kutengeneza fedha

12. Kutoa huduma za kuandikisha majina ya kampuni Je wewe ni mzuri katika kuandika katiba za kampuni unajua jinsi ya kuchagua jina sahihi la kampuni au unajua stepu zinazohitajika ili ukamilishe uandikishe jina la biashara Anza sasa fungua biashara yako ya kutoa huduma za kuandikisha majina ya kampuni .

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

6 Comments
  1. Nimependa maelezo yako natamani nianze biashara moja wapo ambayo haiitaji mtaji.

  2. Hata mimi nasemaga Siku zote Kama mtu unapanga kuanzisha biashara yako basi anza bila kuweka sababu zitakazo kukwamisha katika kuanzisha biashara yako.

  3. Asante sana kwa maelezo ya biashara hizi na mimi nitajitahidi nianzishe moja wapo.

Leave a Reply to Lenald Minja Cancel reply