Aina za Udongo Tanzania

Aina za udongo ni nyingi na Udongo ni rasilimali muhimu sana Tanzania inayotumiwa katika shughuli mbalimbali ikiwemo kilimo ambacho kinategemewa na watanzania kuendesha uchumi wa taifa.

Lakini uharibifu wa mazingira umechangia kushuka kwa thamani ya ardhi na kuathiri kilimo cha mazao, mifugo na uvuvi.

Kutokana na mabadiliko yanayojitokeza kwenye udongo, wananchi wameshauriwa kulima mazao yanayoendana na aina ya udongo uliopo katika eneo husika.

Tanzania ni moja lakini udongo hutofautiana kutoka eneo moja hadi lingine ambapo mazao yanayolimwa hutofautiana katika eneo husika ili kuhakikisha uwiano mzuri wa mazao yanayolimwa nchini.

Aina za Udongo wa Tanzania

  1. Udongo wa Kichanga

Ukanda wa Pwani ambao unajumuisha mikoa ya Dar es salaam na Pwani, sehemu kubwa ya udongo wake ni ya kichanga. 

Udongo wa kichanga huundwa kutokana na kuvunjika vunjika na kumomonyoka kwa miamba kama vile mawe ya chokaa, matale, mawe meupe ya kung’aa na mwambatope.

Udongo huu hauhifadhi maji ambapo maji kupenya kwa urahisi huzuia matatizo ya kuoza mizizi pia Udongo wa kichanga huruhusu maji kupitiliza zaidi ya kiasi kinachohitajika, ambayo husababisha mimea kukosa maji wakati wa kiangazi.

Kutokana na sifa za udongo huo wakulima wanashauriwa kulima mazao yanayohimili ukame kama mihogo, kunde, uwele ambayo huwa mkombozi wakati wa njaa.

  1. Udongo wa Mchangatope

Mchangatope ni udongo wenye chenga ndogo zaidi kuliko udongo wa mchanga hivyo ni laini unapoushika. Udongo huu ukimwagiwa maji, unateleza kama sabuni na unapatikana zaidi katika Nyanda za Juu za Kati mwa nchi.

Huundwa na madini kama vile mawe angavu ambayo yana madini aina ya kwatzi na punje ndogo ndogo za mabaki ya viumbe hai.

Ni chengachenga kama udongo wa mchana lakini unahodhi virutubisho vingi zaidi na unyevu pia Udongo huu una uwezo mdogo wa kuhifadhi maji.

  1. Udongo wa Tifutifu

Udongo tifutifu hutengenezwa na uwiano mzuri wa mchanga, mchangatope, mfi nyanzi na mabaki ya viumbe hai.

Huchukuliwa kama udongo unaofaa zaidi katika ardhi inayolimika. Udongo tifutifu una rangi nyeusi na unafanana na kushika unga mikononi.

Umbile lake ni mchanga mchanga na huhodhi maji kirahisi sana, hata hivyo upenyezaji wake wa maji ni mzuri. Kuna aina nyingi za udongo tifutifu kuanzia wenye rutuba hadi ulio na tope zito na tabaka nene la juu.

Hata hivyo kati ya aina zote hizi tofauti za udongo, udongo tifutifu ndio unaofaa zaidi kwa kilimo.

Kwa Tanzania udongo huu hupatikama zaidi Nyanda za Juu Kusini na Kaskini mwa nchi hasa katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Njombe na Ruvuma.

  1. Udongo wa Mfinyanzi

Udongo mfinyanzi huundwa na chembe chembe ndogo sana ambazo zina sehemu ndogo sana ya kupitisha hewa.

Udongo mfi nyanzi huundwa baada ya miaka mingi ya miamba kumomonyoka na athari za hali ya hali ya hewa.

Mara nyingi vidimbwi hutokea kwenye udongo mfi nyanzi na udongo hugandamizwa kwa urahisi. Kutokana na uwezo wake mdogo wa kupenyeza maji, hatari ya maji kutuama na ardhi kuwa ngumu, sio rahisi kufanya kazi na udongo wa mfinyanzi.

Udongo huu hupatikana zaidi Ukanda wa Kaskazini Magharibi na Nyanda za Magharibi Kigoma na maeneo ya mkoa wa Mwanza.

Subscription Form

Tuandikie email yako uweze kupata post za mtandao wa wauzaji kwa haraka.

Tuandikie Mawazo Yako

Leave a reply

Wauzaji
Logo